Friday, January 30, 2015

KIONGOZI wa tawi la Mpira Pesa la Magomeni jijini Dar es salaam, Ustadh Masoud kwa niaba ya wanachama wenzake amemshutumu makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ kuhusika katika matokeo mabaya ya klabu hiyo katika mechi za ligi kuu Tanzania bara.

Masoud amezungumza leo kuwa wamepata taarifa kuwa Kaburu analipangia benchi la ufundi wachezaji wa kucheza.

“Tumesikia kuwa kiongozi wa juu (Kaburu) anahusika kupanga wachezaji, hii haiwezekani, tukikutana tutajadili hili na kuchukua hatua”. Alisema Masoud.

Alipotafutwa Kaburu amekanusha taarifa hizo na kudai kiongozi huyo lazima aangaliwe sana kwani ana nia mbaya ya kuivuruga klabu.


“Nimemsikia akisema Kaburu anahusika kupanga wachezaji, binafsi nakanusha hilo, uongozi tutamchukulia hatua kwa kumpeleka kamati ya maadili ya klabu”. Amesema Kaburu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video