MABINGWA mara mbili mfululizo wa Tanzania mwaka
1999 na 2000, Mtibwa Sugar wametoka suluhu pacha ya bila kufungana na Mafunzo
ya Zanzibar katika mechi ya mwisho ya kundi C iliyomalizika jioni hii uwanja wa
Amaan Zanzibar.
Mtibwa Sugar wamefikisha pointi tano kufuatia
kushinda mechi moja na kutoka sare mbili.
Mafunzo wao wameshatupwa nje ya mashindano baada
ya kuambulia pointi moja katika mechi tatu ambapo ilichapwa mara na kutoka sare
mechi moja.
Mechi ya kwanza Mafunzo walotandikwa 2-0 na JKU, mechi ya pili wakafungwa bao 1-0
na Simba na leo wameambulia sare.
Usiku majira ya saa 2:15, Mnyama Simba atachuana
na JKU katika uwanja wa Amaan kukamilisha mechi ya hatua ya makundi.
Kama Simba watashinda mechi hiyo watafikisha
pointi 7 kibindoni na kuibuka vinara wa kundi hilo.
Kama timu hizo zitatoka suluhu au magoli, basi
Simba watashika nafasi ya tatu kwa kujikusanyia pointi nne, wakati JKU watakuwa
vinara kwa pointi tano sawa na Mtibwa katika nafasi ya pili, lakini tofauti ni
magoli ya kufunga na kufungwa.
Mpaka sasa Mtibwa wameshafunga magoli mawili na
kufungwa moja, wakati JKU wamefunga magoli matatu na kufungwa moja.
Kwa mujibu wa ratiba kama Simba watakuwa wa tatu
kwa maana ya mshindwa bora watachuana na vinara wa kundi A ambao ni Yanga.
Tayari joto limeshaanza kupanda kwa mashabiki
kwani kuna dalili kubwa ya watani kukutana katika hatua ya robo fainali.
0 comments:
Post a Comment