MAAFANDE wa JKT Ruvu Stars wanaonolewa na beki na
kocha wa zamani wa Yanga, Fredy Felix Minziro ‘Cataraiya Baba Isaya Majeshi’
wameibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Ndanda fc ‘Mtwara Kuchele’ katika
mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara uliomalizika jioni ya leo uwanja wa Azam Complex,
Chamazi, jijini Dar es salaam.
Minziro amesema mechi ilikuwa nzuri, wachezaji
wake walicheza kwa uangalifu na hatimaye wamevuna pointi tatu.
0 comments:
Post a Comment