NAHODHA wa zamani wa timu ya Taifa ya Nigeria,
Super Eagles, Jay Jay Okocha haamini kama golikipa wa timu ya taifa ya nchi
yake, Vicent Enyeama au mchezaji mwingine aliyetajwa anaweza kushinda tuzo ya
mwanasoka bora wa Afrika 2014 isipokuwa Yaya Toure.
“Kwa mimi, Yaya Toure ndiye mshindi asilia.
Nadhani orodha ya wanaowania tuzo inaonesha kuwa kwa miaka mitatu iliyopita,
soka la Afrika halijazalisha nyota wengi kwasababu wachezaji wawili au watatu
wameendelea kuwepo kwa miaka mitano mpaka sita: Yaya Toure, Samuel Eto’o na Didier Drogba.
“Kwasasa
Eto’o na Drogba wametoka na inaonekana Yaya Toure ana nafasi kubwa ya kuendelea
kuwepo. Baada ya yeye, sidhani kama tunazalisha wachezaji nyota Afrika”
Hata hivyo,
Okocha ambaye aliwahi kung’ara katika soka la Afrika hadhani kama nyota
huyo wa kimataifa wa Ivory Coast na timu yake ya Manchester City wanaweza
kutetea ubingwa wa EPL walioshinda mwaka jana.
0 comments:
Post a Comment