MKOMBOZI wa Simba katika mechi ya fainali ya kombe
la Mapinduzi iliyopigwa uwanja wa Amaan usiku huu, Mjini Zanzibar, Ivo Philip
Mapundo amejawa na furaha kubwa baada ya kuisaidia timu yake kutwaa ubingwa kufuatia
kudaka penalti ya Vicent Barnabas iliyowapa ushindi.
Akizungumza kwa furaha na mtandao huu baada ya
mechi kumalizika Ivo alisema: “Mwalimu aliniamini, akaniingiza dakika za
majeruhi kwa lengo la kudaka penalti. Kitu cha kwanza nilichowaza ni
kutokumuangusha mwalimu. Kwali nimefanya vizuri, nina furaha sana”.
Kipa huyo alisema katika siku tatu alizofanya
mazoezi, mwalimu alimuona katika mazoezi ya kudaka penalti na akamwambia kuwa
kama itafikia hatua ya matatu angemtumia.
Pia amewataka wanasimba kuwa na umoja katika
kipindi hiki kizuri kwani kuwa na migongano kutaishusha timu.
“Kikubwa wanasimba wawe na subiri, timu ni nzuri
na tunaamini tutafanya vizuri katika mechi za ligi”. Aliongeza Ivo.
0 comments:
Post a Comment