Floyd Mayweather ndiye bondia anayelipwa zaidi na anajua namna ya kutumia utajiri wake anaopata kwa jasho jingi.
Mfalme huyu wa kuvuna ma-paundi mengi mwaka jana alipata paundi milioni 66.1, hii ni kwa mujibu wa jarida la Forbes.
Nyota huyu wa masumbwi ame-post picha inayoonesha vitu unavyoweza kununua endapo fedha sio tatizo kwako.
Ameonesha magari yake yenye thamani ya paundi milioni 5 na ndege binafsi.
Hata hivyo inaelezwa kuwa mwaka huu anaweza kuvuna mkwanja mrefu zaidi kuliko mwaka jana kama ataamua kupigana na hasimu wake mkubwa Manny Pacquiao.
0 comments:
Post a Comment