Liverpool wamekumbana na maisha magumu zaidi katika msimu wa 2014-15 ikiwemo kipigo cha 3-0 kutoka kwa Manchester United
LIVERPOOL imeanguka msimu huu wa 2014-2015 na ukweli ni kwamba hata kama watashinda mechi zao 17 zilizosalia katika kampeni ya kusaka ubingwa wa ligi kuu England hawataweza kufikisha pointi 84 walizovuna msimu uliopita.
Kikosi cha Brendan Rodgers kilikuwa na makali mno msimu uliopita na kumaliza katika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Manchester City kikifunga magoli 101.
Lakini msimu huu timu imeshuka kiwango ambapo wameshinda mechi 9 na kujikusanyia pointi 32 katika mechi 21 walizokipiga msimu huu...na matokeo hayo yameifanya Liverpool iwe nafasi ya 8 katika msimamo.
Brendan Rodgers yuko katika presha kufuatia kumuuza Luis Suarez kwenda Barcelona.
Kufikia katikati ya januari wakati huu mechi 17 zikisalia, Liverpool haiwezi kufikisha pointi 84 ambazo walipata msimu uliopita.
Kama watashinda mechi zote watafikisha pointi 83.
0 comments:
Post a Comment