Thursday, January 8, 2015

Ibrahim Hajibu akiwa na mpira wake uliopewa jana usiku baada ya kufunga 'Hat-trick'

MFUNGAJI wa mabao matatu ‘Hat-trick’ Simba ikishinda mabao 4-0 dhidi ya Taifa ya Jang’ombe  katika mchezo wa robo fainali ya kwanza ya kombe la Mapinduzi, Ibrahim Hajibu ‘Mido’ alipewa jukumu maalumu la kuwaliza Wazanzibar uwanja wa Amaan Zanzibar jana usiku.

Nyota huyo aliyeingia mapema kipindi cha pili akitokea benchi na kuchukua nafasi ya Elius Maguli aliuambia mtandao huu baada ya mechi kuwa kocha Goran aliona mapungufu ya wapinzani wao, hivyo akampa mbinu ya kwenda kufunga magoli.

“Nimefurahi sana kufunga mabao matatu. Kocha alinipa majukumu ya kufunga, namshukuru Mungu nimefanikiwa”. Alisema Hajibu.

“Kinachosumbua ni nafasi, kila mwalimu anaponipa nafasi lazima nifanye vizuri”.

“Mashabiki wa Simba watarajie mambo mazuri kwani timu inazidi kuimarika”

Nyota huyo alikabidhiwa mpira wake baada ya ‘Hat-trick’ na alifafanua kuwa ni jambo kubwa kwake na kwa Wanasimba wote.

Hiyo ni ‘Hat-trick’ ya pili katika mashindano haya kwani ya kwanza ilifungwa na Saimon Msuva katika mechi ya kwanza ya kundi A Yanga ikishinda mabao 4-0 dhidi ya Taifa ya Jang’ombe.

Taifa ya Jang’ombe imeweka rekodi ya kusababisha ‘Hat-trick’ mbili katika mashindano haya mpaka kufikia hatua hii ya robo fainali.


Pia ndio timu iliyopata kipigo kinachofanana cha mabao 4-0 dhidi ya timu Kurwa na Doto za Kariakoo yaani Simba na Yanga katika mashindano haya.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video