Daniel Sturridge alitua uwanja wa ndege wa Heathrow
Daniel Sturridge yuko mbioni kuonekana kwa mara ya kwanza akiichezea Liverpool baadaye mwezi huu tangu alipoumia mwezi wa nane mwaka jana.
Afya ya nyota huyo imeimarika baada ya kufanyiwa matibabu nchini Marekani.
Mshambuliaji huyo mwenye miaka 25 amekaa nje ya uwanja kwa zaidi ya miezi akiwa na majeruhi ya mguu, lakini kocha Brendan Rodgers amethibitisha kuwa anaweza kurudi mwezi huu.
Sturridge alitua jana mchana uwanja wa ndege wa Heathrow baada ya kufanyia matibabu kwa muda mrefu na madaktari wa Boston Red Sox na daktari binafsi, Scott Schrimscher kwa lengo la kurudi uwanjani.
0 comments:
Post a Comment