Radamel Falcao anataka kubakika Manchester United
HATIMA ya Radamel Falcao kubakia Old Trafford itaamuriwa mwezi Aprili, lakini mshambuliaji huyo ameonesha kutamani kukaa England.
Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa mkopo msimu uliopita kutokea Monaco amekumbana na maisha magumu nchini England-akifunga magoli matatu tu katika mechi 12 za ligi alizocheza-lakini amejijengea mazingira mazuri kwa Louis van Gaal baada ya kufanya vizuri wiki mbili za karibuni.
Kwa sasa Klabu imepata nguvu kuliko awali ya kumpa mkataba wa kudumu Mcolombia huyo anayelipwa paundi laki mbili elfu sitini na tano kwa wiki.
0 comments:
Post a Comment