WAANDAAJI wa tuzo za mchezaji bora wa
Afrika “Glo-CAF Awards” wamethitisha kuwa wanamuziki nyota wa Afrika
watatumbuiza siku hiyo.
Tuzo hizo zitafanyika januari 15 mwaka
huu mjini Lagos, Nigeria ambapo msanii wa juu wa Afrika, Flavour na msanii mkubwa wa Afrika
kusini Hugh Masekela watatoa burudani kali.
Wasanii wa Hip Pop mapacha P-Square nao
watapanda jukwaani baadaye wakati tuzo hiyo ya mchezaji bora ikitolewa ambapo
inawaniwa na wachezaji watano , Vincent Enyeama, Ahmed
Musa,Yaya Toure, Pierre-Emerick
Aubameyang na nyota wa
kimataifa wa Ghana, Asamoah Gyan.
Pia Fally Ipupa, Mwimbaji wa Misri, Hakim; Kikundu maarufu kwa kwaya cha Soweto cha Uhuru;
pan-African group,Cirque Afrique na
mkali wa Bongo Fleva wa Tanzania Diamond ni
baadhi ya wasanii watakaotumbuiza.
Msanii wa Nigeria wa RnB, Wande
Coal, afrobeat Icon, Lagbaja na
Balozi wa Glo, Omawumi nao
watatumbuiza.
0 comments:
Post a Comment