Wakala Jorge Mendes ameshindwa kukanusha uwezekano wa David de Gea kujiunga na Real Madrid
HATIMA ya baadaye ya kipa wa Manchester United, David de Gea katika klabu hiyo imekuwa kitendawili baada ya wakala wake kushindwa kukanusha tetesi za kujiunga na Real Madrid majira ya kiangazi mwaka huu.
De Gea amebakiza miezi 18 katika mkataba wake na bado hajaingia makubaliano ya mkataba mpya ili aendelee kutumika Old Trafford na taarifa za kutua Bernabeu zinazidi kuwa na uzito.
Wakala wake, Jorge Mendes ambaye pia ni wakala wa Cristiano Ronaldo, aliulizwa na vyombo vya habari vya Hispania kama kipa huyo mwenye miaka 24 anaweza kujiunga na Madrid.
De Gea amekuwa katika kiwango cha juu akiichezea Manchester United
0 comments:
Post a Comment