Cristiano Ronaldo anaweza kutimkia Marekani
MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo anaweza kufuata nyayo za David Beckham na Frank Lampard kwa kutimkia Marekani, hii ni kwa mujibu wa wakala wake.
Wakala huyo, Jorge Mendes amesisitiza kuwa Ronaldo, ndiye mchezaji bora wa wakati wote na kuna nafasi ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno kuelekea Marekani mara mkataba wake utakapomalizika Real Madrid mwaka 2018.
Kama ilivyo kwa Steven Gerrard anayekaribia kujiunga na LA Galaxy akiwa na miaka 34, Ronaldo atakuwa nyuma mwaka mmoja ukilinganisha na nahodha wa Liverpool wakati atakapomaliza mkataba wake Madrid na anaweza kufuata nyayo hizo.
Mkataba wa Ronaldo Real Madrid
utamalizika mwaka 2018 wakati ambao atakuwa na miaka 33
0 comments:
Post a Comment