Saturday, January 24, 2015

ALIYEKUWA nahodha wa Simba, Mganda, Joseph Owino amerejea kwao Uganda kwa madai ya kutofautiana na kiongozi mmoja wa juu wa Simba.

Taarifa kutoka chanzo makini zinaeleza kuwa Owino aliingia kwenye mgogoro na viongozi wa Simba Oktoba 25 mwaka jana baada ya kumuamuru kipa kinda Peter Manyika alale chini dakika za majeruhi katika mechi ya ligi kuu Tanzania bara waliyotoka sare ya 1-1- na Tanzania Prisons uwanja wa Sokoine.

Manyika kwa kufuata maelekezo ya nahodha wake Owino,  alilala chini, lakini akajishitukia na kutaka kusimama na ndipo akakutana na mpira wa juu ambao alishindwa kupangua na kufungwa goli rahisi.

Manyika alipoulizwa kwanini alilala, alimjibu kocha Patrick Ackson Phiri na viongozi wa Simba akisema aliaambiwa na Owino alale chini.

Viongozi wa Simba walikasirika ikikumbukwa walikuwa na ugonjwa wa ‘sare sare maua’ na walitaka kuvunja mkataba wa Owino, lakini kocha Phiri alimtetea sana na kusema bado anamhitaji.

Phiri aliwahi kukiri kuwepo kwa mvutano wa Owino na viongozi, lakini alisema kutokana na kumtetea beki huyo wa kati wakakubali kwa shingo upande na kuagiza asajiliwe beki mwingine na ndipo akaletwa Juuko Mursheed.

Viongozi wa Simba hawakutaka Owino acheze, badala yake walihitaji Mursheed na Isihaka wasimame katika ngome ya ulinzi.

Baada ya kuondoka kwa Phiri kumemaliza kila kitu na kuna uwezekano mkubwa Owino asicheze tena Msimbazi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video