Kikosi cha Azam kilichoanza leo
AZAM FC imewalaza bao 1-0 mabingwa watetezi wa
Zanzibar, KMKM, katika mchezo wa kombe la Mapinduzi uliomalizika usiku huu
uwanja wa Amaan Zanzibar.
Huo ni ushindi wa kwanza kwa Azam fc baada ya
kutoka sare ya mabao 2-2 katika mchezo wa awali dhidi ya mabingwa watetezi wa
kombe la Mapinduzi KCCA ya Uganda.
Bao pekee la Azam lilipatikana katika dakika ya 18
kutokana na nahodha wa KMKM, Khamis Ali kujifunga kwa kichwa akijaribu kuokoa
mpira wa krosi uliochongwa na Shomari Kapombe.
Kikosi cha KMKM
Kiujumla timu
zote zilicheza vizuri na kushambuliana kwa zamu, lakini Azam wameonekana kukosa
mipango na kuzua hofu kwa mashabiki wao ikizingatiwa wanaenda kuwakilisha nchi
katika michuano ya ligi ya mabingwa Afrika sanjari na kutetea ubingwa wa
ligi kuu Tanzania bara..
Kocha
mkuu wa Wanalambalamba hao, Mcameroon, Joseph Marius Omog amekiri ugumu wa KMKM
.
"Tulikutana nao
Kigali kombe la Kagame, ni wapinzani wa kweli. Wameimarika, lakini timu yangu
imejitahidi kucheza vizuri". Alisema Omog.
Michuano hiyo itaendelea kesho kwa mechi za mwisho
za kundi C ambapo Mafunzo watakabiliana na Mtibwa Sugar majira ya saa 10:00
jioni uwanja wa Amaan.
Majira ya saa 2:15 usiku katika uwanja huo huo,
Simba watashuka dimbani kuchuana na JKU.
0 comments:
Post a Comment