"Kama klabu, tunazipongeza JKU na Mtibwa
Sigar kwa kushinda na kutinga Nusu Fainali.... tunajua kuwa moyo wa timu yetu
ni kiungo... Tunacheza na viungo ambao ni kama wapya kwenye timu (Domayo,
Mudathir, Majwega na wakati mwingine Erasto) tunawapa muda makocha wetu,
tunajua wanaona matatizo na wanayafanyia kazi.
Wakati mwingine timu hupita kwenye kipindi kigumu
cha majeruhi na kupoteza mtiririko wake.... Katika kipindi kama hiki, muhimu
kama timu ni kukaa pamoja, kujadili matatizo yetu pamoja na kuyafanyia
kazi.
Tunaendelea kuipongeza Mtibwa Sugar na sisi tunabeba changamoto
na kuzifanyia kazi.
Tutasafiri hadi Lubumbashi DRC kucheza na Zesco,
TP Mazembe na Don Bosco katika kuendelea kuiandaa timu. Tumepania kufanya vema
Afrika na tuna imani na makocha wetu.
Kama walifanya vizuri wakiwa na KCCA na AC
Leopards kwa nini wasirudie mafanikio hayo wakiwa na sisi.
Azam FC, Tucheze pamoja kwa furaha”
0 comments:
Post a Comment