Beki wa Celtic, Virgil van Dijk (katikati) amefungua milango ya kwenda EPL
DILI la Arsenal kumnunua Virgil van Dijk linaweza kukamilika kufuatia beki huyo wa Celtic kuonesha nia ya kuzungumza na klabu za ligi kuu England, EPL kama zitatoa ofa mwezi huu.
Celtic wanasisitiza kuwa hawataki kumuachia beki huyo labda kama kutakuwa na dau kubwa, lakini Van Dijk ametaja umri wake kuwa sababu kubwa ya kuhitaji kuondoka.
"Kwasasa nimeanza kuwaza kuhusu hilo (maisha ya baadaye)," Van Dijk aliwaambia De Telegraaf.
"Nina umri wa miaka 23 sasa na nimecheza Willem II, FC Groningen na Celtic na sasa nahusishwa na klabu kama Arsenal. Sio jambo kubwa?
"Kuna klabu nyingi zinavutiwa na mimi, lakini Celtic wanaweka ngumu wakitaka ada kubwa ya usajili. Klabu ipo sawa: hawataki kuniachia majira ya baridi kwasababu tunacheza makombe manne.
0 comments:
Post a Comment