Ame alipokuwa anafanya mahojiano maalumu na mwandishi wetu mchana wa leo
MSHAMBULIAJI hatari wa Mtibwa Sugar, Mzanzibar,
Ame Ally 'Zungu' anasumbuliwa na wanawake wengi wakati huu jina lake linavuna katika
soka la Tanzania.
Akizungumza na mtandao huu katika Hoteli ya
Bwawani Mjini Zanzibar ambapo Mtibwa imeweka kambi, Ame amesema kabla hajawa
maarufu wanawake hawakumsumbua, lakini tangu aanze kupata fedha za mpira
imekuwa shida kwake.
“Lalalala! ‘mademu’ wanasumbua sana! Lakini mimi
nina akili. Najiuliza mbona wakati sina kitu hawakuwa wengi, sahizi nina kitu
wanasumbua, hawa wanataka vitu tu wala hawana mapenzi ya kweli” Alisema Ame.
Ame aliongeza kuwa yeye ni baba wa mtoto mmoja
anayeitwa Amina.
“Nimeoa
na nina mtoto mmoja wa kike anaitwa Amina, kila ninachofanya ni kwaajili ya
mwanangu, nafikiria sana maisha yake ya baaday e,hivyo ni lazima nijitume sana
na kumuomba Mungu” Amesema Ame Aly.
Akizungumzia penati aliyoikosa katika mchezo wa robo
fainali dhidi ya Azam FC, Ame amekubali kuwa huwa hana bahati na kufunga penati
toka nyuma lakini amesema kuwa, hakuna mjanja katika penati hivyo ili uweze
kufunga lazima uwe na mazoezi ya mara kwa mara.
0 comments:
Post a Comment