YANGA imethibitisha kushiriki michuano ya kombe la
Mapinduzi inayotarajia kuanza kutimua vumbi januari Mosi mwakani.
Makamu mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga amesema
mwaka jana hawakupeleka timu Zanzibar, kitendo ambacho kilitafsiriwa vibaya na
Wazanzibar mpaka walipoenda kuomba msamaha.
Sanga amesema hawataki tena kurudia makosa, hivyo
watapeleka kikosi cha kwanza katika michuano hiyo.
Wakati huo huo nao Mabingwa watetezi wa ligi kuu
Tanzania bara, Azam fc wamethibitisha kupeleka kikosi cha kwanza katika
michuano ya Mapinduzi.
Afisa mtendaji mkuu wa Azam fc, Sady Kawemba amesema michuano hiyo
ni fursa kwao kuendelea kujiandaa na michuano ya ligi na ligi ya mabingwa
Afrika.
Taarifa zinaeleza kuwa wapinzani wa Azam katika
ligi ya mabingwa Afrika, Al Merreick ya Sudan nao wanaomba kushiriki michuano
hiyo.
0 comments:
Post a Comment