IMERIPOTIWA kuwa beki wa zamani wa Simba na
Coastal Union, Juma Nyosso amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Mbeya City.
Taarifa zinaeleza kuwa Nyosso aliyekaa bila timu
kwa miezi mitano tangu aachane na Wagosi wa Kaya tayari alishatua Mbeya kuanza
kazi.
Afisa habari wa Mbeya City, Dismas Teni alisema
taarifa rasmi ya nani amesajiliwa na nani ameachwa itatolewa desemba 10 mwaka
huu mara baada ya kikosi cha timu hiyo kurudi Mbeya kutokea Songea-Ruvuma.
Wagonga nyundo hao wa Mbeya waliwasili jana Mjini Songea
ambapo wanatarajia kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya JKT Mlalale na Maji
Maji FC zinazoshiriki ligi daraja la kwanza na watakipiga na vinara wa ligi kuu
Mtibwa Sugar ya Morogoro.
0 comments:
Post a Comment