BEKI wa kushoto wa Simba SC, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’
amesema kuna changamoto kubwa kukipiga timu kongwe na zenye mashabiki lukuki.
Akizungumza
na mtandao huu katika mazoezi ya Simba yanayoendelea maeneo ya Chang’ombe
Dar es salaam, Tshabalala amesema Simba ni timu kubwa yenye wachezaji wengi,
lakini anajituma katika mazoezi kuhakikisha kuwa anaendelea kumshawishi bosi
wake Patrick Phiri.
“Kuna changamoto ya kiuchezaji, Simba ni timu
kubwa. Najituma kuhakikisha naendelea kucheza katika kikosi cha kwanza”.
Alisema Tshabalala.
“Malengo yangu ni kufika mbali, napenda sana
kuondoka hapa nilipo na kwenda kucheza soka la kulipwa nje ya nchi”.
0 comments:
Post a Comment