MSHAMBULIAJI wa Hispania, Fernando
Torres amekubaki kurudi kwa mkopo Atletico Madrid kutokea klabu yake ya sasa ya
AC Milani mpaka mwishoni mwa msimu wa 2015-16, hii ni kwa mujibu wa taarifa
iliyotolewa leo na mabingwa hao wa La Liga.
Torres atarudi katika klabu yake hiyo
aliyokulia ikiwa imepita miaka saba na nusu.
Nyota huyo mwenye miaka 30 amekumbwa
na ukame wa magoli tangu alipojiunga na Chelsea kutoka Liverpool mwaka 2011 na
alienda kwa mkopo AC Milan mwezi wa nane mwaka huu.
Chelsea na Milan zilikubaliana
jumamosi kufanya usajili wa kudumu na kutoa mwanya kwa Torres kujiunga na
Atletico kwa mkopo ambapo ataanza kujijenga upya chini ya kocha mwenye mvuto
klabuni hapo, Diego Simeone.
0 comments:
Post a Comment