MFUNGAJI bora wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu
uliopita, Amiss Tambwe amesema anaweza kutetea kiatu chake cha dhahabu kwani
ligi bado ‘mbichi’.
Tambwe ambaye anaendelea kujifua katika mazoezi ya
timu yake ya Simba amesema yeye malengo yake ni kufunga ingawa changamoto
imeongezeka kwake.
“Mpaka sasa nina goli moja tu, lakini nikicheza
mechi tatu zijazo nina uhakika wa kufunga mabao mawili mawili. Najiona kuwa
fiti zaidi kutokana na mazoezi ya Gmy tuliyofanya na yanayoendelea sasa”.
Alisema Tambwe.
Nyota huyo aliyefunga mabao 19 msimu uliopita
aliongeza kuwa mashabiki wa Simba waendelee kuwaunga mkono kwani sasa
wanajipanga kuwafurahisha zaidi baada ya kupitia kipindi cha mpito.
0 comments:
Post a Comment