Zacharia Hans Poppe
KAMATI ya usajili ya Simba imeshindwa kupata beki
wa kati kama walivyoagizwa na kocha mkuu, Mzambia, Patrick Phiri.
Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba sc,
Zacharia Hans Poppe ameuambia mtandao huu kuwa kocha Phiri aliagiza apatikane
beki wa kati wa kiwango cha juu, lakini wameshindwa kupata beki wa aina hiyo
katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili.
Poppe aliongeza kuwa inabidi kocha aendelee na
mabeki waliopo kwa sasa.
Kepteini huyo wa zamani wa JWTZ aliongeza kuwa
kocha aliagiza apatikane mshambuliaji mkali na wamefanikiwa kumsainisha miaka
miwili nyota wa Gor Mahia ya Kenya, Mganda Danny Sserunkuma.
Aidha aliongeza kuwa wapo katika mazungumzo ya
mwisho na nyota wa Polisi Morogoro Danny Mrwanda na Hassan Kessy wa Mtibwa Sugar.
Muda wowote kutoka sasa makubaliano na wachezaji
hao yatafikiwa na kuwasainisha mikataba.
0 comments:
Post a Comment