Goran anatua kesho nchini kusaini mkataba wa kuifundisha Simba
RAIS wa Simba SC, Evans Elieza Aveva leo
anatarajia kukutana na kocha mkuu wa klabu hiyo, Patrick Ackson Phiri
kumtaarifu juu ya kufutwa kazi kufuatia kutoridhishwa na mwenendo wa timu hiyo
katika michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara.
Simba wameshinda mechi moja, wamefungwa moja na
kutoa sare mechi sita, hivyo kujikusanyia pointi 9 katika nafasi ya 10 ya
msimamo.
Phiri (kushoto) na Matola (kushoto) wamefukuzwa kazi
Wakati huo huo, kocha Mserbia Goran Kapunovic
anatua kesho jijini Dar es salaam kusaini mkataba wa kuifundisha klabu hiyo na
taarifa zinaeleza kuwa anatasaidiwa na Mnyarwanda Jean Marie Ntagwabira.
Kwa maana hiyo naye msaidizi wa Phiri, Seleman
Matola ‘Veron’ anaondoshwa katika nafasi yake, ingawa yeye atapelekwa Simba B
kwa lengo la kukuza vipaji.
0 comments:
Post a Comment