Kocha Mkuu wa Simba Patrick Phiri (kushoto) akiwanoa vijana wake
KOCHA mkuu wa Simba sc, Patrick Phiri amesema
kikosi chake kinazidi kuimarika kutokana na mazoezi ya nguvu wanayoendelea
kuyafanya kwa sasa kujiandaa na raundi ya nane ya ligi kuu soka Tanzania bara
na mechi ya Nani Mtani Jembe 2.
Akizungumza katika mazoezi ya Simba yanayoendelea
kufanyika uwanja wa JKT Mbweni jijini Dar es salaam, Phiri alisema baada ya
kutoka mazoezi ya Gmy ameona mabadiliko ya vijana wake na wanatia matumaini
kuelekea mechi zijazo.
Mzambia huyo aliongeza kuwa lengo ni kuhakikisha
idara zote zinakuwa na nguvu ya kutosha, lakini anaangalia zaidi sehemu ya
ushambuliaji kwani mpaka sasa timu hiyo haijafunga mabao mengi.
“Kusajiliwa kwa Sserunkuma (Danny) ni jambo nzuri
sana. Nimemuona mara kadhaa akiichezea timu yake ya Taifa (Uganda). Ni mchezaji
mahiri. Wakikaa na Okwi (Emmanuel) na Tambwe (Amiss) nadhani tutakuwa na safu yenye ubora”.Alisema Phiri.
Kuelekea mechi ya nani Mtani Jembe itakayopigwa
Desemba 13 mwaka huu, Phiri alisema maandalizi yanakwenda vizuri na anafurahi
kukutana na Yanga.
“Itakuwa mechi nzuri. Yanga ni wapinzani wetu
wakubwa na timu kubwa nchini, tunaendelea kujipanga na tunaamini kuibuka na
ushindi”.
“Nawashukuru sana mashabiki wetu, wamekuwa nasi
kwa wakati wote. Sasa ni muda wa kuwafurahisha”.
Simba leo inatarajia kucheza mechi ya kimataifa ya
kirafiki dhidi ya The Express ya Uganda katika uwanja wa Taifa na jumapili
itakipiga na Mtibwa Sugar katika uwanja huo.
Baada ya mechi hizo, Mnyama anatarajia kuweka
mawindo yake visiwani Zanzibar kuitafuta mwarobaini Yanga .
0 comments:
Post a Comment