MANUEL Pellegrini amewashutumu
wachezaji wake wa Manchester City kwa kuwaruhusu Burnley kusawazisha mabao yote
mawili waliyokuwa wanaongoza na kulazimishwa sare ya 2-2.
Mabingwa hao watetezi walipoteza
nafasi ya kuwasogelea kwa karibu vinara wa ligi kuu, Chelsea ambao walibanwa
mbavu na Southampton mapema jana jumapili.
“Labda kuongoza 2-0 tulidhani mechi
imeisha, lakini mpaka kipyenga cha mwisho mpira unakuwa bado haujamalizika.
Hatukuendelea na kasi ile ile”
“Katika mpira, mipira miwili tu inaweza
kuamua matokeo. Mwanzoni kwa kipindi cha pili, Burnley walifunga goli la
kuotea, baada ya pale, walifunga bao la mpira kwa mpira uliorudi uwanjani baada ya kugonga mwamba”
0 comments:
Post a Comment