KIUNGO bora wa ulinzi wa Simba SC, Jonas Gerard
Mkude amesema wachezaji wengi wa kitanzania wana malengo ya kucheza soka la
kulipwa, lakini hawajitumi kutengeneza njia.
Mkude ambaye siku za hivi karibuni alisaini
mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia Simba alisema kila mchezaji
akiulizwa malengo yake anasema anataka kwenda ulaya, lakini jitihada za kwenda
huko hazionekani.
“Unaweza kusema nina malengo ya kwenda ulaya,
lakini ukawa unacheza hapa hapa tu kwasababu hujitumi. Kinachotakiwa kwa sisi
wachezaji ni kujiongeza zaidi kimazoezi ili kuwa fiti kwa changamoto za
kimataifa”. Alisema Mkude.
“Nina ndoto za kwenda kucheza soka la kulipwa,
lakini inabidi nijitume hapa nilipo ili kusonga mbele”.
Mkude ambaye ni kipenzi kikubwa cha mashabiki wa
Simba aliongeza kuwa kikosi chao ni bora na wamekuwa wakishangaa pale
wanaposhindwa kupata matokeo.
“Ujue matokeo yaliyokuwa yanapatikana yanashangaza
sana. Si kocha, wachezaji, viongozi, wala mashabiki, wote hatuelewi kwanini
inakuwa hivyo wakati tuna timu nzuri” Alisema Mkude.
Kuhusu kocha Phiri, Mkude alisema ni ‘bonge’ la
kocha kwani mara zote anakuwa kama mzazi.
“Mbali na kuwa kocha, Phiri ni kama mzazi, anawapenda
wachezaji, anapenda kuelekeza, kifupi ni kocha mzuri sana. Viongozi na
mashabiki wampe muda”. Alisema Mkude.
0 comments:
Post a Comment