MSHAMBULIAJI hatari wa Polisi Morogoro, Danny
David Mrwanda amakiri kumaliza mazungumzo na viongozi wa Simba juu ya yeye
kujiunga na timu hiyo wakati huu wa dirisha dogo la usajili.
Mrwanda amesema makubaliano yamefikiwa na imebaki
kwa upande wa Simba kutekeleza matakwa yake ili ajiunge na wekundu hao wa
Msimbazi.
Nyota huyo wa zamani wa Taifa Stars na Simba
tayari yupo jijini Dar es salaam kusikilizia mpango huo na kama mambo hayataenda
sawa anatarajia kutua nchini Vietnam kucheza soka la Kulipwa.
“Kwasasa nipo hapa Dar es salaam, kuna mambo
nayamalizia. Kweli nimezungumza na Simba, kilichobaki ni wao kutekeleza
makubaliano”. Alisema Mrwanda alipohojiwa na mtandao huu.
Mrwanda ni miongoni mwa wachezaji waliopendekezwa
na kocha mkuu wa Simba, Patrick Phiri katika ripoti yake baada ya mechi saba za
ligi kuu Tanzania bara.
Katika mechi sita zilizopita, Simba ilipata sare
zote na kushinda moja.
Simba imeanza mazoezi ya Gym na uwanjani maeneo ya
Chang’ombe jijini Dar es salaam.
0 comments:
Post a Comment