MSHAMBULIAJI mwenye kipaji kikubwa, Mganda Hamis
Friday Kiiza ametua nchini leo kudai barua ya kuthibitishwa kuachwa na Yanga.
Kiiza ambaye hakuwahi kuiangusha Yanga katika
mechi kubwa hasa dhidi ya Mtani wake Simba amesema hana kinyongo na klabu yake
ya Yanga na anaiheshimu sana.
Nyota huyo aliyekataliwa na kocha aliyefukuzwa
Yanga, Marcio Maximo amesema baada ya taarifa za kuachwa na Yanga, Simba
walizungumza na wakala wake wakihitaji kumsajili, lakini hakuwa tayari
kwasababu alikuwa anaiheshimu klabu yake.
Kiiza amesema amepata timu nzuri (hajaitaja) ana
atasaini ndani ya wiki saba zijazo.
0 comments:
Post a Comment