KIUNGO wa ulinzi wa Simba, Jonas Mkude anaendelea
vizuri na anaweza kurudi ndani ya siku mbili au tatu atarudi uwanjani.
Mkude aliugua ghafla jana usubuhi katika kambi ya
Simba iliyopo Ndege Beach Hotel maeneo ya JKT Mbweni nje kidogo ya jiji la Dar
es salaam.
Daktari wa Simba, Yassin Gembe aliuambia mtandao
huu kuwa Mkude aliugua marelia na alipelekwa hospitali.
“Mkude ni kweli amepata marelia. Lakini si kubwa
sana, siku mbili au tatu atarudi uwanjani”. Alisema Gembe.
Kwa upande wake Mkude ambaye alipumzika hotelini
wakati wa mazoezi ya jana jioni alisema anaendelea vizuri, hivyo mashabiki
wasiwe na wasiwasi.
0 comments:
Post a Comment