KIPA namba moja wa
Simba SC, Ivo Mapunda amerejea mazoezini baada ya kumzika mama yake mzazi Bi
Igasia Nchimbi wiki iliyopita.
Kipa huyo wa zamani wa
Yanga, Saint George ya Ethiopia na Gor Mahia ya Kenya aliingia mazoezini katika uwanja wa JKT Mbweni akiwa na gari
binafsi.
Ivo ambaye alionekana
kutokuwa na furaha kutokana na matatizo yaliyomkuta alikuwa anarudisha kasi
yake sambamba na kipa kinda Peter Manyika Jr.
“Sipo vizuri kutokana
na machungu niliyonayo, lakini nimerudi kazini kuendelea na mazoezi”. Alisema
Ivo.
0 comments:
Post a Comment