BEKI anayeaminiwa kwa sasa na kocha wa Simba sc, Patrick
Phiri, Hassan Isihaka amesema kuwa
kujiamini, kujituma na kuwa na subira ndio siri ya mafanikio yake ya
sasa.
Isahaka amesema amepita mikononi mwa makocha
tofauti Simba SC, lakini amekuja kuaminiwa na kocha wa sasa.
“Nimehangaika sana, nakumbuka kuna wakati
nilitolewa kwa mkopo kwenda Africa Lyon. Kocha kama Logarusic (Zdravko)
hakuniamini kabisa. Alivyokuja Phiri nikajiamini na kuonesha kile nilichokuwa
nacho”. Alisema Isihaka.
“Loga hakuwaamini vijana, lakini Phiri ni kocha
anayetutia moyo na kutufanya tucheze mpira kwa kujiamini”
Beki huyo ambaye amecheza mechi zote saba za ligi
kuu Tanzania bara aliongeza kuwa anajitahidi kukwepa kufanya makosa yasiyokuwa
ya lazima ingawa mpira wa miguu ni mchezo wa makosa.
Aidha alisema kuwa malengo
yake ni makubwa na anataka kuisadia kwanza Simba msimu huu halafu mambo mengine
yatafuata.
0 comments:
Post a Comment