Cholo mwenye jezi namba mbili
NAHODHA na
beki wa kulia wa Simba SC, Masoud Nassor
‘Cholo’ amesema kwasasa yuko fiti kabisa na hana majeruhi ya aina yake.
Cholo ambaye anashiriki mazoezi ya Simba kwa
asilimia 100 alisema kuwa ana furaha ya kurudi uwanjani na haogopi ushindani wa
namba katika kikoso hicho.
“Nimetoka kwenye majeruhi. Ukweli ni kwamba siwezi
kuwa fiti kama awaili, lakini najituma kurudisha kasi yangu”. Alisema Cholo.
Kwa kipindi ambacho Cholo hakuwepo uwanjani nafasi
yake ya unahodha ilikuwa chini ya Mganga Joseph Owino ‘Gella’.
0 comments:
Post a Comment