Cholo akiwa Gym kufanya mazoezi
NAHODHA wa Simba, Masoud Nassor ‘Cholo’ kwasasa
yuko fiti kucheza mechi ya aina yoyote.
Daktari wa Simba, Yassin Gembe ameuambia mtandao
huu kuwa afya ya Cholo ambaye amerithiwa unahodha na Joseph Owino imeimarika kwa
asilimia mia moja kufuatia kusumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara.
“Cholo yuko fiti kucheza hata kesho. Hivi
tunavyozungumza alikuwa kambi ya timu ya taifa ya Zanzibar kujiandaa na
michuano ya CECAFA Challenge”. Alisema
Gembe.
Baba Ubaya akiwa mazoezini
Daktrai huyo aliongeza kuwa beki wa kushoto wa
klabu hiyo ambaye amesumbuliwa na majeruhi kwa muda mrefu sasa, Issa Rashid
‘Baba Ubaya’ naye amepona majeraha yake.
“Issa (Rashid) yuko fiti pia. Ameanza mazoezi na
yuko tayari kwa mechi”. Alisema Gembe.
Kuhusu Paul Kiongera, Gembe alisema kuwa
mshambuliaji huyo raia wa Kenya amemaliza muda wake wa mapumziko, lakini bado
ni majeruhi na hawezi kusema atarudi uwanjani siku gani.
“Kiongera hali yake bado kabisa, kwahiyo siwezi
kusema ni lini atakuwa tayari kucheza”. Alisema Gembe.
Wekundu wa Msimbazi Simba wanaendelea na mazoezi
mara moja kwa siku ambapo wanaanzia Gym na kumalizia katika uwanja wa TCC
Sigara Chang’ombe Dar es salaam.
0 comments:
Post a Comment