MSHAMBULIAJI huru Betram Mwombeki amesaini mkataba
wa mwaka mmoja kuitumia klabu ya Ruvu Shootings ya Pwani inayoshiriki ligi kuu
soka Tanzania bara.
Nyota huyo wa zamani wa Simba ameanza mazoezi na
kikosi cha Shootings kinachonolewa na kocha Mkenya, Tomy Alex Olaba.
Mazoezi hayo yanafanyika katika kambi iliyopo
Mabatini Mlandizi mkaoni Pwani.
Msemaji wa klabu hiyo, Masau Bwire amethibitisha
taarifa hiyo jioni ya leo na amesema bado kocha Olaba yupo katika mawindo ya
kuongeza nyota wengine.
Bwire amesema kwa sasa hawawezi kutaja wachezaji
wanaotakiwa na kocha huyo aliyewahi kuifundisha kwa Mtibwa Sugar ya Morogoro.
0 comments:
Post a Comment