Wednesday, November 12, 2014

Kamati ya Mpira wa Miguu wa Vijana ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeunda jopo la watu watano kuhakiki umri wa wachezaji watakaoshiriki hatua ya ngazi ya Taifa ya michuano ya Copa Coca-Cola 2014.

Michuano hiyo ya ngazi ya Taifa itafanyika Dar es Salaam kuanzia Desemba 13 hadi 20 mwaka huu. Uhakiki wa umri utafanyika Desemba 11 na 12 mwaka huu wakati timu zote zinatakiwa kuwasili Shule ya Filbert Bayi mkoani Pwani kuanzia Desemba 10 mwaka huu.

Jopo hilo la uhakiki linaongozwa na Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Henry Tandau. Wengine katika jopo hilo ni Ally Mayay, Charles Boniface Mkwasa, Dk. Jonas Tiboroha na Richard Yomba.

Timu 16 zitakazocheza michuano hiyo inayoshirikisha watoto wenye umri chini ya miaka 15 ni Arusha, Dodoma, Geita, Katavi, Kigoma, Kinondoni, Kusini Pemba, Kusini Unguja, Lindi, Mbeya, Mjini Magharibi, Morogoro, Mwanza, Ruvuma, Simiyu na Tanga.

Vyama vya mpira wa miguu vya mikoa vinakumbushwa kutuma TFF fomu za usajili ambazo zinatakiwa kuambatanishwa vyeti vya kuzaliwa vya wachezaji husika.


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video