Friday, November 14, 2014

OKTOBA 18 mwaka huu, Dar Young Africans ilichuana na mahasimu wake wa jadi, Simba Sports Club  katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam.

Mechi hii ilikuwa na mvuto wa aina yake kutokana na matokeo ya mechi za nyuma kwa timu zote.

Simba waliingia uwanjani wakiwa na kumbukumbu ya sare tatu katika mechi tatu za mwanzo ambapo walianza ligi kwa kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Coastal Union, wakalazimishwa sare ya 1-1 mara mbili dhidi ya  Polisi Morogoro na Stand United.

Mnyama aliingia kwa hesabu za kutafuta pointi tatu za kwanza mbele ya mtani wake wa jadi na wakaamua kujificha nchini Afrika kusini kusaka makali.

Hata hivyo kambi hiyo iliyowekwa ‘Bondeni kwa Mzee Madiba’ haikuwasaidia vijana wa Patrick Phiri kuifunga Yanga.

Yanga wao waliingia uwanjani wakiwa tayari wameshaonja ladha ya ushindi mara mbili, ingawa walianza kwa kutandikwa mabao 2-0 na Mtibwa Sugar katika mechi ya ufunguzi wa ligi kuu iliyopigwa septemba 20 mwaka huu uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.
Yanga walishinda mabao 2-1 mara mbili dhidi ya  Maafande wa Tanzania Prisons ‘wajelajela’ na JKT Ruvu.
Mechi ya Yanga na Simba ilihudhuriwa na mashabiki lukuki, lakini ilimalizika kwa suluhu pacha ya bila kufungana.

Timu zote zilicheza kwa umakini, ufundi na nguvu, lakini washambuliaji wa timu zote walishindwa kutumia nafasi walizopata.
Rekodi  iliyowekwa baada ya matokeo hayo ni timu hizo kongwe kutoka sare katika mechi zao tatu za ligi kuu zikiwa na makocha tofauti.

Msimu  uliopita mzunguko wa kwanza, Simba na Yanga zilitoka sare ya mabao 3-3.

Yanga walianza kufunga mabao 3-0 kipindi cha kwanza, lakini Simba walikuja juu kipindi cha pili na kusawazisha yote.

Wakati huo, Simba ilikuwa chini ya kocha mkuu Alhaj Abdallah Athuman Seif maarufu kwa jina la King Abdallah Kibadeni akisaidiwa na kocha mwenye maneno mengi, Jamhuri Kiwhelo ‘Julio’.

Yanga wao walikuwa chini ya kocha Mholanzi, Ernie Brandts akisaidiwa na Fred Felix Minziro.

Mzunguko wa pili timu hizo zilitoka sare ya 1-1, Simba ikiwa chini ya kocha Mcroatia, Zdravko Logarusic ‘Loga’ akisaidiwa na Selemani Matola na Yanga ilikuwa chini ya Mholanzi Hans van Der Pluijm akisaidia na Charles Boniface Mkwasa.


Msimu huu mechi ya mzunguko wa kwanza timu zimetoka suluhu,  Simba wapo chini ya kocha Mzambia Patrick Phiri akisaidiwa na Matola wakati Yanga inanolewa na Mbrazil Marcio Maximo akisaidiwa na Mbrazil mwenzake Leonardo Neiva.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video