Monday, November 10, 2014

Wakati Azam wakicheka uwanja wa Taifa, Dar Young Africans walikuwa na kibarua kizito kuwakabili maafande wa Mgambo JKT Katika dimba la Taifa, Dar es salaam.
Mechi hiyo iliyotawaliwa na rafu nyingi ilimalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Wachezaji wa timu zote walioneshana ubabe wa hapa na pale, lakini mara kadhaa mwamuzi Ngole Mwangole kutoka Mbeya alipeta.

Hata hivyo, Mgambo walilazimika kucheza pungufu kwa dakika 38 baada ya mchezaji wao Salum Hamis Kipaga kuoneshwa kadi nyekundu kufuatia kumpiga kiwiko Mrisho Ngassa.
Naye Mbuyu Twite alimpiga teke Fuluzulu Maganga wa Mgambo akilipiza kisasi kufuatia kufanyiwa madhambi, lakini mwamuzi Ngole Mwangole kutoka Mbeya alimuonesha kadi ya njano.

Kitendo hicho kilizua utata ambapo mashabiki, wachambuzi na makocha wa mpira walidai kuwa Twite alistahili kadi nyekundu.
Mbali na matukio hayo, Malimi Busungu alijikuta akioneshwa kadi ya njano akidaiwa kujiangusha, lakini picha za marudio zilionesha dhihiri  kuwa aliangushwa na beki wa Yanga.
Licha ya kuwa pungufu, Mgambo JKT walishambulia lango la Yanga, lakini kipa Deo Munish alijitahidi kuonesha umahiri wake kwenye milingoti mitatu.

Nao Yanga walijizatiti kuhakikisha wanapata magoli na katika dakika ya 73, Saimon Msuva akitokea benchi aliandika bao la kuongoza akimalizia mpira mrefu wa Mbutu Twite.

Dakika za majeruhi, Msuva aliandika bao la pili akimalizia mpira uliookolewa na beki wa Mgambo kutokana na purukushani za Hassan Dilunga.


Ilionekana Dilunga amemfanyia madhambi mlinda mlango wa Mgambo, lakini haikumzuia mwamuzi kukubali goli hilo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video