JIJINI Dar es salaam kulikuwa na mchezo mkali baina
ya Simba na Ruvu Shootings ya Pwani.
Mechi hii
ilivuta hisia za mashabiki wengi kutokana na mfululizo wa matokeo ya sare sita
kwa wekundu wa Msimbazi Simba.
Mnyama
Simba ilianza kwa kasi kulisakama lango la Ruvu Shootings wakisaka bao la
kuongoza.
Mara kadhaa
Amissi Tambwe, Emannuel Okwi na kiungo Said Ndemla walikosa nafasi nzuri za
kuandika magoli.
Naye beki
wa kati Joseph Owino alikuwa anapanda kuongeza kasi ya mashambulizi, lakini
dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika kwa suluhu ya bila kufungana.
Kipindi cha
pili Tambwe na Okwi waliokenaka kuwa na kasi kubwa wakisaka goli, lakini mabeki
wa Ruvu Shooting walikuwa makini kuokoa.
Simba hawakukata
tamaa hata kidogo kwani walijua wazi kuwa mashabiki wa timu hiyo wana hamu ya
ushindi.
Mashabiki
wachache waliokaa jukwaa la Yanga waliendelea kuwakebehi wachezaji wa Simba na
mashabiki wake.
Lakini
Elias Maguri aliyetokea benchi aliwachachafya mabeki wa Ruvu Shootings na
katika dakika ya 77 aliingia eneo la hatari na kupiga mpira uliokolewa na kipa
wa Shootings na Emmanuel Okwi alimalizia na kuwainua vitini mashabiki wao.
Katika
mechi sita za mwanzo, Simba walikuwa wanafunga mabao katika kipindi cha kwanza
na kurudishwa kipindi cha pili.
Walitangulia
kwa mabao 2-0 dhidi ya Coastal Union, lakini yakasawazishwa kipindi cha pili.
Walitangulia
kwa bao 1-0 dhidi ya Polisi Morogoro, lakini likasawazishwa kipindi cha pili.
Walitangulia kwa bao 1-0 dhidi ya Stand United, likasawazishwa kipindi cha
pili.
Mechi ya
watani wa jadi dhidi ya Yanga hawakufungana, lakini katika mechi dhidi ya
Prisons walitangulia kwa bao 1-0, lakini likasawazisha na katika mechi na
Mtibwa walitangulia bao 1-0, likasawazishwa kipindi cha pili.
Mechi ya
mwishoni mwa wiki hawakufunga goli kipindi cha kwanza na kundi la UKAWA
liliingia uwanjani na kuonesha kidole kimoja juu wakimaanisha timu inashinda
1-0 na ikatokea hivyo.
0 comments:
Post a Comment