Mechi nyingine iliyoingia kwenye rekodi ya pekee ni
baina ya Mtibwa Sugar iliyopigwa uwanja wa Manungu Complex Oktoba 8 na 9 mwaka
huu.
Kinachovutia zaidi ni mechi hii kuchezwa kwa siku
mbili yaani Oktoba 8 ilipigwa kwa dakika 45 na kuahirishwa kufuatia mvua kubwa
kunyesha na maji kujaa uwanjani.
Katika dakika hizo, Mtibwa Sugar waliibuka na
ushindi wa bao 1-0.
Siku ya pili mechi hiyo ilichezwa kwa dakika 45 za
kipindi cha pili na Kagera wakaibuka na ushindi wa bao 1-0.
Hivyo mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya bao 1-1 na
hii ni rekodi ya aina yake.
0 comments:
Post a Comment