Friday, November 14, 2014

Mechi nyingine iliyoweka rekodi mpaka kufikia raundi ya saba ni ile ya Mgambo JKT dhidi ya Mbeya City fc iliyopigwa uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga oktoba 3 mwaka huu.

Awali mechi hii ilipangwa kuchezwa Oktoba 2 mwaka huu, lakini kutokana na mvua kubwa iliyonyesha Tanga, uliahirishwa kufuatia uwanja kujaa maji.
Mbeya City fc waliokuwa na hamu ya kushinda baada ya kufungwa mechi mbili mfululizo, bao 1-0 dhidi ya Azam fc na mabao 2-0 na Mtibwa Sugar uwanja wa Sokoine walijikuta wakifungwa mabao 2-1 na Mgambo.

Wakiendelea kujiuliza nini kimetokea, wakajikuta wakifungwa tena 1-0 na Stand United, Oktoba 8 mwaka huu uwanja wa CCM Kambarage Shinyanga.

Rekodi iliyowekwa na Mbeya City msimu huu ni kufungwa mechi nne mfululizo na kushika mkia katika msimamo wa ligi kuu ikijikusanyia pointi tano tu.

Pia ni timu pekee iliyofunga mabao mawili tu, tena moja la penati ya Deogratius Julius kwenye mechi dhidi ya Coastal Union iliyochezwa septemba 27 mwaka huu uwanja wa Sokoine Mbeya.


Deus Kaseke aliifungia bao la pili msimu huu katika kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Mgambo JKT.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video