Wednesday, November 12, 2014

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imepitisha usajili wa Ligi Daraja la Pili (SDL) huku ikikata majina mawili ya wachezaji katika klabu za Abajalo ya Dar es Salaam na Magereza ya Iringa.

Klabu hizo mbili zilisajili wachezaji 31 badala ya 30 ambapo ni kinyume na Kanuni ya 61(2) ya Ligi Daraja la Pili inayoruhusu klabu kusajili wachezaji wasiozidi 30 na wasiopungua 18.

Wachezaji ambao Kamati ya Sheria iliyokutana jana (Novemba 11 mwaka huu) imewaondoa ni wale waliokuwa wameorodheshwa namba 31 katika usajili wa klabu hizo. Wachezaji hao ni Andrew Mathew Kazembe (Abajalo) na Joshua Omari (Magereza).

Michuano ya Ligi Daraja la Pili inayoshirikisha timu 24 katika makundi manne ya timu sita kwa mtindo wa nyumbani na ugenini itaanza kutimua vumbi Novemba 22 mwaka huu.

Wachezaji waliopitishwa katika kila klabu na idadi yao kwenye mabano ni Abajalo (30), Arusha FC (18), Bulyanhulu (28), Kariakoo (30), Kiluvya United (23), Magereza (30), Mbao (27), Milambo (29), Mji Mkuu (29) na Mkamba Rangers (30).

Wengine ni Mpanda United (29), Mshikamano (28), Mvuvumwa (18), Njombe Mji (25), Pamba (24), Rwamkoma JKT (25), Singida United (26), Town Small Boys (22), Transit Camp (28), Ujenzi Rukwa (30), Volcano (25) na Wenda (20).


Klabu zote zinakumbushwa kulipia na kuchukua leseni za wachezaji wao kabla ya ligi kuanza, kwani kwa mujibu wa kanuni hakuna mchezaji atakayeruhusiwa kucheza mechi ya ligi bila kuonyesha leseni yake. 

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video