Mechi nyingine ilipigwa uwanja wa Chamazi Complex, Dar es salaam ambapo JKT Ruvu
waliwakaribisha Ndanda fc.
Kikosi
hicho cha Fredy Ferlix Minziro kiliibuka na ushindi wa mabao 2-0 ambapo mabao
hayo yalifungwa na Najimu Magulu na Samuel Kamutu.
Hata hivyo
timu zote zilishambuliana kwa zama, lakini JKT Ruvu wakaweza kuvuna pointi tatu
muhimu.
Baada ya
kukamilika kwa raundi ya saba ya ligi kuu soka Tanzania bara, msimamo umekuwa
hivi.
Ligi kuu
itasimama kwa zaidi ya mwezi mmoja na siku kadhaa kupisha mechi ya kirafiki ya
kalenda ya FIFA baina ya Swaziland na Tanzania itakayopigwa Novemba 15 mwaka
huu.
Pia
kutakuwepo na michuano ya mataifa ya Afrika mashariki na kati, CECAFA Senior
Challenge Cup na michuano ya vijana chini ya miaka 20, Uhai Cup 2014.
Pia
kutakuwa na dirisha dogo la usajili ambapo makocha wa timu zote watatumia
nafasi hiyo kuongeza makali.
0 comments:
Post a Comment