Tuesday, November 4, 2014

Hassan Isihaka (kulia). Picha na Bin Zubeiry

BEKI anayezidi kukonga nyoyo za Wanamsimbazi, Hassan Isihaka amesema matokeo ya sare wanayozidi kupata yanawaumiza mno na hawaelewi kwanini inakuwa hivyo.

Isihaka aliongeza kuwa kwa wakati wote wachezaji wamekuwa tayari kucheza, wanajituma, wanafunga magoli, lakini yanarudi kirahisi tu.

“Unajua hata sisi hatuelewi kwanini inakuwa hivi. Tunafanya vizuri, lakini tunaishia kupata sare. Nakwambia inatuuma sana na hatuelewi kwanini inakuwa hivi”. Alisema Isihaka.

Mlinzi huyo mahiri ambaye alifanya makosa mechi iliyopita na kuwapa mwanya Mtibwa Sugar  kusawazisha goli alisema kuwa wakati wote anajitahidi kutekeleza majukumu yake na kukwepa kufanya makosa, lakini mpira wa miguu ni mchezo wa makosa.

Pia alimsifu kocha wa Simba Patrick Phiri kuwa ni kama baba mlezi.


“Kocha Phiri ni mzuri sana. Anaishi na sisi kama Baba Mlezi. Anajua kuelekeza, ana mbinu nzuri, uongozi ungempa muda zaidi, naamini tutafanikiwa kufanya vizuri zaidi”. Alisema Isihaka.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video