Tuesday, November 18, 2014

MLINDA mlango namba mbili wa Simba sc, Hussein Sharrif ‘Casilas’ ameanza mazoezi leo baada ya kutoa nyuzi alizoshonwa kwenye ugoko kufuatia kuumia katika mazoezi ya Mnyama yaliyofanyika nchini Afrika kusini mwezi uliopita.

Casillas ameanza mazoezi ya Gym na kukimbia mchangani baada ya kufungua nyuzi  za chuma alizoshonwa.

Kipa huyo bora wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu uliopita anaanza mazoezi ya peke yake na anaamini Mungu atamjaalia afya njema ili arudi uwanjani.

Casillas aliumia Oktoba 11 mwaka huu, Simba ikicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Orland Pirates  nchini Afrika kusini iliyomalizika kwa suluhu ya bila kufungana.

Kipa huyo aligongwa ugoko kwa njuma za chuma na mshambuliaji wa miamba hiyo ya Afrika kusini.

Kwasasa Simba inamtegemea zaidi kipa namba tatu, Peter Manyika Jr kwani hata kipa namba moja Ivo Mapunda hajawa fiti kwa asilimia 100.

Wakati huo huo kuna taarifa kuwa Simba inataka kumrudisha kipa wake wa zamani anayecheza Yanga, Juma Kaseja katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili.


Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe alisema katikati ya wiki iliyopita kuwa Kaseja yuko huru kurudi Simba kwani ni sawa na nyumbani kwake.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video