Monday, November 10, 2014

Uwanja wa Chamazi Complex ambapo Mabingwa watetezi, Azam fc walichuana vikali na mabingwa wa Tanzania mwaka 1988, Coastal Union ya Tanga.

Mechi hii ilivuta hisia za mashabiki wengi kwasababu Azam fc waliingia uwanjani wakiwa na kumbukumbu ya kutandindwa  bao 1-0 katika mechi mbili mfululizo dhidi ya JKT Ruvu Uwanja wa Chamazi na Ndanda fc uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mkoani Mtwara.

Kabla ya kipyenga  kupulizwa kuashiria kuanza kwa kipute hicho, kiungo mahiri wa Azam fc, Salum Abubakary maarufu kama ‘Sure Boy’ alizawadiwa ‘mkwanja’ wa shilingi milioni moja ikiwa ni zawadi ya mchezaji bora wa mwezi kutoka kwa wadhamini wa ligi, kampuni ya Vodacom Tanzania.
Kipindi cha kwanza, Azam fc waiingia kwa kasi wakilisakama lango la wapinzani wao na katika dakika ya 6, mshambuliaji aliyekosekana katika vipigo viwili, Kipre Herman Tchetche alipiga shuti kali lililogonga mtambaa panya.

Azam waliendelea kulisakama lango la Coastal, lakini mlinda mlango mahiri Shaaban Hassan Kado alijitahidi kuokoa michomo kadhaa ya hatari.

Kipindi cha pili, Azam waliendelea kushambulia wakisaka bao la kuongoza, lakini mabeki wa Coastal walijitahidi kupambana.

Dakika ya 55, Wagosi hao wa Kaya walishambulia lango la Azam kama nyuki, lakini kipa Aishi Salum Manula alifanya kazi ya ziada kuiokoa timu yake.

Timu zote ziliendelea kushambuliana kwa kasi na katika dakika ya 84 Azam waliandika goli la kuongoza kupitia kwa Kipre Tchetche.


Dakika tano baadaye, Shomari Kapombe aliandika bao la pili, lakini dakika za majeruhi, Rama Salim aliiandikia Coastal bao la kufutia machozi kwa mpira wa adhabu ndogo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video