Tuesday, October 7, 2014

Na Francis Kivuyo

Ukitaja taasisi zenye nafasi na nguvu kubwa katika jamii, huwezi kuwacha kutaja Makanisa na Misikiti. Misikiti na Makanisa zimekuwa na msaada mkuwa sana katika jamii katika kufundisha masuala ya kiroho lakini pia wakifundisha mambo muhimu ya kijamii ikiwemo maendeleo kama vile; Kilimo, Elimu  pamoja na uongozi bora kwa kutaja vichache tu.

Kama Misikiti na Makanisa zimefanikiwa kutengeneza na kuendeleza miradi mikubwa ndani na nje ya nchi; mfano ujenzi wa shule, mahosipitali na mabenki, basi taasisi hizi zinauwezo mkubwa wa kuchangia kwa namna moja ama nyingine katika maendeleo ya soka letu.
Kwa mfano; Misikiti na Makanisa  zina nafasi nzuri ya kujenga vituo vya soka (football academy) kubwa na za kisasa  kwa ajili ya kuwajenga vijana wetu kiafya, kimaadili na kuwatengenezea njia nzuri ya ajira mbeleni kwa kuwa michezo ikiwemo mpira wa miguu ni ajira sasa hivi kwa vijana wengi. Nasema hivyo kwa sababu, taasisi hizi zinaaminika kuwa na umoja na ushirikiano mkubwa, wakisema wafanye kitu siyo rahisi kurudi nyuma.

Kwa maana hiyo ni mategemeo yangu kwamba  shirikisho la kandanda nchini, TFF chini ya raisi Jamal Emil Malinzi litalitazama suala hili kwa mtazamo chanya kuona ni jinsi gani wanaweza wakashirikiana na taasisi zetu za kidini katika kulisasaidia  soka la vijana wetu kwa maendeleo yetu sisi wenyewe. Hata kama hawataweza kujenga vituo vya soka lakini, bado wanaweza wakawa wanatia mikono yao katika hiyo program maalumu ya soka la vijana ambayo ipo chini ya TFF.
Tukifanya hivyo, naamini  mpango wa kutengeneza vipaji vya soka  kuanzia ngazi ya chini itawezekana tena kwa mafanikio makubwa na kwa  muda mfupi tofauti na kuwaachia shirikisho peke yao kulifanya.

Tukitumia nchi ya Uingereza kama mfano, kuna timu zinazoshiriki ligi kuu nchini humo  ambazo chimbuko lao ni makanisani; mfano Everton FC ambayo iliundwa na kanisa la Methodist la mtakatifu Domingo mwaka 1878 na inajaribu kufanya vizuri katika ligi mbalimbali za nchini Uingereza. Mfano mwingine ni timu ya Bolton Wanderers ambayo inamilikiwa na kanisa pia.

Kama hawa wamefanya na wamefanikiwa kwa kiasi hicho, kwa nini sisi tusiweze? Tunaweza sana, kikubwa ni TFF kutengeza mahusiano mazuri na ya karibu na taasisi za kidini ambayo itawafanya kutengeneza mipango kama hiyo ambayo tunaamini itakuwa na msaada mkubwa katika kuendeleza soka letu. 

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video