Saturday, October 11, 2014



Na Frank Momanyi Mgunga, Dar es salaam

WAKATI timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars ikitarajiwa kushuka ugani hapo kesho katika mtanange wa kukata na shoka dhidi ya timu ya taifa ya Benin mchezo utakaopigwa katika dimba la uwanja wa taifa jijini Dar es salaam, baadhi ya wadau wa soka nchini wamesema wana imani na timu hiyo kuwa itapeperusha vyema bendera  ya Tanzania katika  mchezo wa hapo kesho.

Akiongea na MPENJA BLOG,  mchezaji wa zamani wa klabu ya Yanga Seklojo Chambua amesema mchezo wa hapo kesho ni kiwango sahihi kwa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro premium lager chini ya kocha Mholanzi Mart Nooij ambaye anapenda kutumia mfumo wa 4-3-3, lakini je mfumo huo utaweza kuizamisha Benin ?

Chambua alisema mfumo wa kocha sio kigezo cha kuifanya timu yoyote kuweza kuibuka na ushindi bali juhudi binafsi za wachezaji zinaweza kuipa ushindi timu yoyote ile duniani.

‘’Mfumo wa kocha sio kigezo cha kuifanya timu yoyote kuweza kuibuka na ushindi  bali juhudi binafsi za wachezaji na ushirikiano ndio unaweza  kuipa ushindi timu yoyote ile duniani, kwa hiyo wachezaji wanatakiwa kujituma hapo kesho ili kuhakikisha wanaipa ushindi Taifa”. Alisema Chambua.

Kwa upande mwingine Chambua alisema wingi wa mashabiki katika mchezo  wa kesho itakuwa ni chachu kwa timu ya taifa kuweza kuibuka na ushindi.


Stars ambayo inashuka dimbani ikiwa na  kumbukumbu ya kipigo kutoka kwa timu ya taifa ya Msumbiji na kuweza kuondolewa katika mitanange ya kufuzu michuano ya kombe la mataifa barani Afrika, hapo kesho itashuka ugani ikiwategemea wachezaji wake mahili wanaocheza soka la kulipwa , Thomas ulimwengu, Mwinyi Kazimoto pamoja na Juma Luizio anayekipiga katika klabu ya Zesco fc ya nchini Zambia.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video