Wednesday, October 15, 2014

HOFU imeanza kupungua katika klabu ya Simba SC kufuatia kipa namba moja wa klabu hiyo, Ivo Philip Mapunda kuanza mazoezi mjini Johannesburg nchini Afrika kusini ambako klabu hiyo imewaka kambi kujiwinda na mechi ya watani wa jadi dhidi ya Yanga itayopigwa Oktoba 18 mwaka huu uwanja wa TaifA, Dar es salaam.

Ivo aliyeumia kidole katika mazoezi ya Simba zaidi ya wiki mbili zilizopita mjini Zanzibar alioneka kuwa fiti, hivyo kuwatia moyo wachezaji wenzake.

Joto lilizidi kupanda Msimbazi kufuatia kipa aliyetegemewa kucheza mechi hiyo, Hussein Sharrif ‘Casillas’ kuumia ugoko na katika mazoezi ya jana hakushiriki kabisa.

Kurejea kwa Ivo kutaliweka lango la Simba katika mikono salama kwasababu Peter Manyika asingeweza kuhimili presha ya mechi hiyo.

Kabla ya kwenda Bondeni, Ivo aliuambia mtandao huu kuwa Simba inazidi kuiamarika na wana matumaini ya kufanya vizuri mechi zijazo kuanzia ya Yanga.

“Mashabiki wasife moyo, tulianza kwa sare tatu. Mengi yanazungumzwa, lakini hakuna haja ya kushikana uchawi, kikubwa ni kujiandaa na tunaamini tutaweza kufanya vizuri”. Alisema Ivo.

Aidha, aliongeza kuwa kama Casillas atasimama langoni haitakuwa na tatizo kwasababu ni kipa mzuri, lakini atahitaji kujiamini zaidi kwasababu hajawahi kucheza kwenye mechi ya presha kama hiyo.


Simba ipo kambini nchini Afrika kusini na inatarajia kurejea siku moja kabla ya mechi ya jumamosi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video